Jumamosi, 16 Mei 2015

WATOTO WAFA KISIMANI



SIMANZI na vilio vilitanda katika familia ya mwalimu John Frayo baada ya watoto wao wawili Lucas John(4) na Emmanuel John (2.5)  kutumbukia ndani ya kisima cha maji na kupoteza maisha.
Akizungumza tukio hilo, Diwani wa kata ya Kisarawe 2, Issa Zahor alisema lilitokea jana saa sita mchana mtaa wa Vumilia Ukooni,  wilaya ya Temeke mkoa wa Dar es Salaam ambapo watoto hao walitumbukia katika kisima chenye urefu wa futi tatu kilichopo nyuma ya nyumba waliokuwa wakiishi.
“Watoto walikuwa wakicheza na bahati mbaya walitumbukia katika kisima kilichopo mita 50 nyuma ya nyumba waliokuwa wakiishi na familia,” alisema Zahor.
Alisema kuwa baada ya kuwatoa walikimbizwa hospitali ya Vijibweni,  daktari wa zamu alithibitisha kuwa tayari walikuwa wamekwisha kufariki.
Zahor alisema kuwa kutokana na matukio kama haya kujirudia ameamua kuitisha kikao cha viongozi wa serikali za mitaa ili kujadili namna ya kuepuka vifo hivyo.
“Tukio hili ni la pili ndani ya mwezi mmoja tumepoteza watoto wanne ambao wangekuwa ni nguvu kazi ya Taifa baadae, nimepanga kuitisha kikao cha ODC tuongelee jinsi tutaa,”

  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni