ASKARI wa Jeshi
la Wananchi Tanzania(JWTZ) Lugalo, Barnabas Mataja(48) amefariki dunia baada
kusombwa na maji katika mto Mzinga.
Akithibitisha
kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani ACP Japhari Mohamedi
alisema tukio hilo lilitokea Mei 11 katika eneo la Kimbangulile,Kata ya
Tambani, Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.
Mohamedi
alisema juzi marehemu alikuwa akirudi nyumbani kwake akitokea matembezini wakati akivuka mto huo maji yalimzidi nguvu na
kusombwa.
“Mwili wa
marehemu umepatikana jana saa nne asubuhi katika eneo la Tambani,”
alisema Mohamedi.
Alisema
mwili wa marehemu umechukuliwa na ndugu zake kwa ajili ya maandalizi ya maziko.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni