UTARATIBU
wa kusafirisha mahujaji wanaokwemda nchini Saudi Arabia katika mji mtakatifu
wa Makha kwa mwaka huu umebadilishwa na wizara ya hija ya nchi hiyo.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam Rais wa taasisi ya kusafirisha mahujaji ya AL jazzira international
Hajj trust Alhaj Seifu llah alisema Serikali ya nchi hiyo imeamua
kuboresha mapokezi ya wageni wanaokwenda hija tofauti na zamani.
Alisema
kuwa mahujaji wote wanaokwenda kuhiji taarifa zao zinatakiwa zipatikane
mapema kupitia mfumo maalum wa kielotronik kupitia Paspoti zao ili ijulikane
idadi ya mahijaji wanaoingia nchini humo kwa mwaka huu.
Alisema
lengo la kutaka taarifa hizo mapema na kujua idadi yao ni kutaka kuboresha
maandalizi ya mapokezi kwa mahujaji hao ili waongeze huduma katika maeneo
watakayofikia.
Seifu aliwataka wale wote walikaohitaji
kusafiri wajitokeze mapema kujiandikisha katika taasisi watakazo safari nazo
ili kuepuka usumbufu ambao usio wa lazima.
“Wizara
hiyo imetoa siku ya juni 27 mwaka huu kuwa siku maalumu ya kuufunga mfumo huo
hivyo hujaji yeyote atakaechelewa siku hiyo atakuwa si miongoni mwa watakaosafari.
Alisema
kuwa kwa mwaka huu taaasisi yake ina mpango wa kusafirisha mahujaji kwa njia
ya Gari kupitia Sudani endapo hali ya usalama nchini humo itakuwa ya kuridhisha.
Kwamwaka
huu Al jazira itasafirisha mahujaji kwa dola za kimarekani 4400 na kuhiji kwa
niaba ya mtu asiyejiweza ni dola 1500 hiyo inajumuisha pamoja na gharama zote
kwa siku watakazo kuwa huko.
Hata
hivyo aliwataka mahujaji wanaosafiri na taasisi hiyo kulipia katika benki za
NMB kwa akaunti namba 20410001982 kwa watakaolipia kwa kutumia fedha za
kitanzania na kwa watakaotumia dola za kimarekani akaunti namba 20410002001.
Ibad.
a ya hija kwa waislamu ni moja kati ya nguzo tano ya dini hiyo
|
Jumamosi, 9 Mei 2015
UTARATIBU MPYA WA KWENDA HIJA
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni