BAREGU
Mhadhiri wa Chuo cha Mtakatifu Augustino(SAUT),
Profesa Mwesigwa Baregu amesema hali iliyojitokeza jana ya jaribio la mapinduzi
nchini Burundi ilionekana ingeweza kutokea tangu awali kutokana na msimamo wa
Rais Nkurunziza kuanza kuleta machafuko na uvunjifu wa amani.
Alisema viongozi wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki(EAC) wanatakiwa kuendelea na jitihada zao za kumtaka Rais
Nkurunziza kuachana na msimamo wake na kuhakikisha kuwa utawala wa Jeshi
haujiandai kuota mizizi.
“Hali hii ilionekana inaweza
kutokea…wanachopaswa kufanya viongozi wa EAC ambao nafikiri wataendelea na
mkutano na rais Nkurunziza, ni kuhakikisha kuwa wanaleta suluhu mapema kwa
kuweka serikali ya umoja wa kitaifa ili uongozi wa Kijeshi usijiandae kuota
mizizi na uruhusu uchaguzi kufanyika kama ilivyopangwa, ” alisema Profesa Baregu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni