KESI ya kumtesa mfanyakazi wa ndani inayomkabili mkazi wa
Mwananyamala Amina Maige (42), imeahirishwa katika Mahakama ya Wilaya ya
Kinondoni jana kutokana na mshtakiwa kuvamiwa na watu wasiojulikana na kumkata kwa
mapanga.
Shauri hilo litakuja tena Juni 16, mwaka huu endapo hali ya
mshtakiwa ikiendelea vizuri.
Mbele ya Hakimu Yohana Yongolo, Wakili upande wa Jamhuri
ulidai kwamba shauri hilo lipo mbele ya mahakama hiyo kwa ajili ya kuendelea
kusikilizwa ushahidi upande wa
mlalamikaji.
Mdhamini wa pili wa mshtakiwa Chausiku Maige, aliiambia
mahakama hiyo kwamba Amina ameshindwa kufika mahakamani kwa kuwa alivamiwa na
watu wasiojulikana ambapo tukio hilo lilitokea nyumbani kwake Mei 7, mwaka huu.
“Mheshimiwa mtuhumiwa kwa sasa yupo katika Hospitali ya
Taifa ya Muhimbili Taasisi ya Mifupa (MOI) akiendelea na matibabu baada ya
tukio hilo lililotokea nyumbani kwake alfajiri wakati akitoka ndani kuelekea
kazini.
“Tulitoa taarifa katika kituo cha Polisi Osterbay kisha
tulipewa RB/7647/2015. Amina amepata majeraha makubwa sehemu za mkononi pamoja
na kichwani,” alidai Chausiku.
Hakimu alimuhoji mtuhumiwa huyo kama eneo analoishi mtuhumiwa huyo ana
uhasama na jirani zake, ambapo shahidi huyo alijibu kuwa hajui kwa kuwa anaishi
mbali na mtuhumiwa.
Kwa mara ya kwanza, Amina Maige alipandishwa kizimbani
katika Mahakama hiyo Juni 13, mwaka jana akikabiliwa na tuhuma za kumchoma pasi
na kumng’ata mfanyakazi wake wa ndani Yusta Kashinde (20) hali iliyosababishai
maumivu makali mwilini.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni