MEYA wa Manispaa
ya Ilala, Jerry Silaa ametoa mpya baada
ya kuwataka akina mama wasiwakimbie
wenzi wao wakati huu wa baridi kwa sababu wanajenga hospitali maalumu ya mama
na mtoto.
Hospitali
hiyo itakayokuwa na vitanda 200, itajengwa eneo la Chanika kwa msaada wa watu
wa Korea.
Akizungumza
mwishoni mwa wiki na wakazi wa Mtaa wa Mbondole kata ya Msongola, Meya huyo
alisema msaada huo aliuomba mwenyewe na kwamba wakati wowote kuanzia sasa
ujenzi huo utaanza.
Alisema tayari
mkandarasi kampuni ya CM Multiworks, amepewa kazi ya kujenga zahanati ya
Mbondole ambayo itagharimu Sh milioni 35.
“Naona wakazi wa huku ni hodari sana maana
kila ninayemuona ana mtoto, hivyo kipupwe cha mwaka huu mambo yote mwisho
Chanika…akinamama msiwakimbie kina baba,” alisema Silaa.
Awali Diwani
wa Kata ya Msogola, Angelina Malembeka, alisema eneo la ujenzi wa zahanati ya
Mbondole lenye ukubwa wa hekari mbili, limetolewa na mmoja wa wakazi wa mtaa
huo Hussein Katundu.
“Tunamshukuru
aliyekubali kutoa eneo lake kwa ajili ya ujenzi huu naomba watu wengine muige
mfano huu kwa kutoa maeneo yenu kwa ajili ya huduma za jamii,” alisema.
Aalisema
wakati mwingine, gharama za kununua eneo huwa kubwa kuliko gharama za ujenzi wa
zahanati husika hivyo akashauri watu wengine wajitolee ili kusaidia jamii.
Alisema
zahanati hiyo itakapokamilika kutaifanya kata hiyo kuwa na zahanati tatu.
Zanahati nyingine ni Mvuleni na Kiboga.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni