WATU nane
wameripotiwa kufariki dunia kutokana na mvua zinazo endelea kunyesha katika jiji la Dar es salaam.
Taarifa
iliyotolewa na Kamishna wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam Suleiman Kova,
alisema watu tano wametambuliwa na wengine watatu bado hawajatambulika na miili
yao imehifadhiwa katika ya Hospitali ya
Mwananyamala.
Alisema Mei 6 mwaka huu mnamo saa 1 usiku maeneo ya
magomeni Wilaya ya Kinondoni
aliyetambulika kwa jina Shabani Idd(73) mkazi wa Manzese alisombwa na
maji ya mto ng’ombe alipokuwa akijaribu kuvuka mto huo na mwili wake ulipatikana Mei 7 akiwa
amefariki.
“Kifo
kingine kili tokea Mei 7 mwaka huu mnamo
saa 6 mchana maeneo ya Mwanamnyamala
mbuyuni Masumbuko Douglass (50) alianguka na kufariki dunia ghafla
wakati akitoa maji yaliyo ingia ndani kwake uchunguzi wa awali unaonyesha alikuwa na tatizo la ugonjwa wa kifafa hivyo
wakati akiangaika kutoa maji ugonjwa huo ulimpata na kuanguka kwenye maji”alisema Kova
Alisema
Rashidi Hassan(36) Mkazi wa Mvuruhana Pemba mnazi Kigamboni alizama katika
mkondo wa maji unaoelekea baharini Mei 6 mwili wake ulipatika Mei 7 ukiwa
unaelea majini umbali wa Mita 500 toka eneo alilozama.
“kifo
kingine kimetoke Yombo Makangarawe Mei 6 mtoto Gloria Mrema mwenye umri wa
mwaka moja na miezi mitatu alipotea baada ya watoto wenzake kumuacha wakati
wakicheza kwa pamoja juhudi za kumtafuta zilifanyika bila mafanikio hadi mwili
wake ulipopatikana ukiwa unaelea majini katika mto Mzinga akiwa tayari amepoteza maisha mwili wake umehafadhiwa
Hospitali ya Temeke”alisemaKova.
Alisema kifo
kingine kilitokea Mei 8 mwaka huu Kinondoni Mkwajuni mtu mmoja mwanaume jina
lake hali kufahamika anakadiwa kuwa na umri(40-45) alikutwa amefariki dunia mwili
wake umehifadhiwa Hospitali ya Muhimbili kwa uchunguzi.
“Pamoja na
vifo hivyo kuripotiwa pia mtu mmoja
Mabula Moses(65) mkazi wa vingunguti buguruni Wilaya ya Ilala amevunjika mguu
wake wa kulia chini ya goti baada yakuangukiwa na ukuta wa ghala la Fida Hussen
lilopakana na nyumba yake, majeruhi amepelekwa katika Hospitali ya Amana”alisema.
Alisema katika
Kata ya Mchikichini taarifa ya mafuriko inaonyesha nyumba takribani 70
zimefunikwa na maji hadi juu ya paa ambapo wakazi wake tayari wamehama huku
watu 35 wamejihifadhi Shule ya Sekondari
Mchikichini.
“ Kata
yaJangwani zipo nyumba takribani zinakadiliwa kuwa 100 zimefunikwa namaji hadi
juu ya paa watu 300 walihama mapema.
“Maeneo
mengine yaliyo athirika zaidi kutokana
na mvua hizo ni Keko, Changombe maduka mawili ,Yombo vituka, Vingunguti ,
Africana,Msasani bonde la mpunga,Jangwani ,Manzese, Kigogo, Mburahati, Boko basi
haya na maeneo mengine taarifa hazijapokelewa,”alisema Kova.
Alisema wananchi wote kuchukua tahadhari ya hali ya
juu hasa wale wanaoishi kwenye maenea ambayo ni mikondo ya maji au watumiaji wa
barabara zinazopitiwa na mikondo hiyo.
tuwasaidieni waathirika
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni