Jumatano, 13 Mei 2015

jambazi afyatua risasi na kujeruhi



MTU mmoja ambaye jina lake halikufahamika amepigwa risasi mbili na kuporwa fedha na mtu mmoja anayedhaniwa kuwa ni jambazi katika eneo la  Karibu na Deluxe Bar, Sinza Kijiweni wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo limetokea leo,  katika maeneo hayo ambayo blog hii ilifika na kuelezwa kwamba tukio hilo lilitokea majira ya saa sita mchana.
 Dereva aliyekuwa akiendesha gari lililoshambuliwa lenye namba T 236 DDT alifahamika kwa jina moja la Abbasi alielezea tukio hilo kwa kusema kuwa fedha ambazo majambazi hao walichukua walikuwa wamezitoa benki moja iliyoko Mlimani City.
Dereva huyo anasema kuwa baada ya kuchukua fedha ambazo hakuzitaja zilikuwa kiasi gani lakini watu waliokuwa hapo walisema zilikuwa milioni 10, walitoka Mlimani City na kuelekea katika hospitali ya mtaalamu wa watoto iliyopo Sinza.
“Baada ya kuingia na kuegesha gari alitufuata mtu mmoja aliyekuwa amevalia koti jeusi akiwa ameshuka kwenye pikipiki aina ya Boxer na alipofika alisogelea gari letu na kufunua koti lake, lililokuwa na silaha aina ya SMG,” alisema.
Abbasi alisema kuwa mtu huyo alimuelekezea silaha abiria aliyekuwa nyuma ya gari na kumuamuru kutoa fedha, amri ambayo haikutekelezwa na mtu huyo aliyemueleza kwamba hana fedha.
Abbas alisema baada ya kuona anabishana nae alimpiga risasi ya kwanza, akageuza SMG kwangu nikakimbia, akafyatua lakini hakunipata ndipo nikasikia risasi nyingine ikipigwa,” alisema.
Aliongeza kuwa wakati anarudi alikuta majambazi hao walikuwa wameshaondoka na mkoba wa fedha ‘Briefcase’ na kutokomea nao.
Hata hivyo tukio hilo la kushtukiza liliwafanya wasamalia wema pamoja na wananchi kumpeleka majeruri huyo hospitali .
Ingawa kulikuwa na taarifa kwamba fedha zilizoporwa zilikuwa milioni 10, lakini Dereva huyo alisema kuwa majambazi hao waliondoka na kiasi ambacho hata hivyo hakikuwekwa wazi.
Askari polisi walifika katika eneo hilo na kuzoa kipande cha utumbo kilichokuwa kimedondoka sakafuni kikiwa na maganda matano ya risasi.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni