Jumatatu, 6 Julai 2015

SOKO LA KISUTU KUWA LA KISASA ZAIDI



HALMASHAURI ya Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam imesema imedhamilia kulifanya soko la Kisutu kuwa la kisasa kwaajili ya kikudhi mahitaji ya watumiaji.
Hayo yalielezwa jana na aliyekuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa wakati alipokuwa akivunja  Baraza la Madiwani wa Manispaa hiyo.
Alisema tayari Manispaa hiyo imesaini mkataba na Benki ya Rasilimali(TIB) kwaajili ya kujenga soko la kisasa la Kisutu, kwani licha ya manispaa hiyo kuwa na masoko 18 lakini bado hayoko kwenye ubora unaostahili.
“Manispaa licha ya kuwa na masoko 18 lakini matano t undo makubwa huku huku kwenye hayo matano kukiwa na hilo la Kisutu ambalo tumedhamilia liwe la kisasa kwani liko katikati ya Mji, ” alisem Silaa.
Kwa upande mwingine Slaa alisema kuwa Baraza hilo limevunjwa huku kukiwa na mambo mengi ya kujivunia hususan katika kuandaa mazingira endelevu ya Uwekezaji.
“Kama Manispaa pia tumefanikiwa kuongeza mapato ya ndani, Uboreshaji wa Huduma za Kiuchumi, Elimu na Afya, yote hiyo ikiwa ni kwakushirikiana vizuri na madiwani wote,  ” alisema Silaa.
Silaa pia ametangaza adhma yake ya kutaka kugombea nafasi ya ubunge kwenye jimbo la Ukonga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
 “Ni imani yangu kuwa mwakani mungu akijaalia nitakuwa nanyi kwenye baraza hili lakini nikiwa kwenye nafasi nyingine ya Ubunge, kwani kama walivyoniamini wananchi wa kata ya Gongo la Mboto kuniteua kuwa Diwani wao basi hata kwenye ubunge kazi itakuwanyepesi,” alisema Slaa.
Mwisho                               


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni