Jumatatu, 6 Julai 2015

HUKUMU YA MBASHA YAPIGWA KALENDA



MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala Juni 13, mwaka huu itaeleza iwapo mwimbaji na mfanyabiasha Emmanuel Mbasha ana kesi ya kujibu au la.
Mwendesha Mashtaka Munde Kalombora alisema kwamba mahakama itaeleza baada ya kupitia hoja za pande zote mbili.
Mbasha ambaye ni Mume wa mwimbaji maarufu wa muziki wa injili nchini, Flora mbasha anakabiliwa na tuhuma za ubakaji.
Kesi hiyo inasikilizwa mahakamani hapo na hakimu Flora Mjaya na mwendesha mashtaka Munde kalombora.
"Mara ya mwisho tarehe ilipangwa Julai 4 kimakosa kwani siku hiyo ni jumamosi, leo ( jana) mbasha alikuja isipokuwa mawakili wake, ndio maana Hakimu amepanga waje Julai 13, ili iamuliwe", alisema Munde.
katika kesi hiyo Mbasha anadaiwa kumbaka binti mwenye umri wa miaka 17 ambaye ni shemeji yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni