Jumatatu, 6 Julai 2015

REFSO WASAIDIA KISIMA TAMBANI



TAASISI ya kijamii ya Rehema Friendship  and Solidarity Trust(REFSO) yenye makao yake Mbezi beach jijini Dar es Salaam imewaondolea kero ya maji iliyokuwa ikiwakabili wa wakazi wa kijiji cha Tambani, Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani kwa kuwachimbia kisima kirefu kitakachowasaidia kupata maji bure na karibu.
Akizungumza katika ufunguzi wa kisima hicho, kiongozi wa Taasisi ya REFSO, Mirzagha Mehraliyev alisema kuwa wamekuwa wakitoa misaada mbalimbali kwa jamii ya kitanzania hasa maeneo ya vijijini.
“Tumewafikia idadi kubwa ya watanzania kwa tukichimba visima virefu vya maji na mpaka sasa tuna visima 130 Tanzania nzima ambavyo vimeanza kutumika,” alisema Mehraliyev.
Alisema kisima hicho ambacho kimegharimu kiasi cha tsh.milioni 15 zilizotokana na wafadhiri kutoka Uturuki.
Alisema kuwa jamii inayoishi vijijini inakabiliwa na changamoto nyingi mojawapo ni ukosefu wa maji safi na salama hivyo wao kama watoa misaada wameamuma kuwasaidia wakazi wa kijiji hicho.
Alisema mbali na uchimbaji wa visima, REFSO hutoa misaada mbalimbali zikiwemo huduma za afya, elimu na mambo ya kijamii.
Awali akisoma risala katika ufunguzi huo, mwakilishi wa kijiji hicho Mmembu Saidi aliishukuru Taasisi hiyo kwa kuwaondolea kero hiyo ambayo ilikuwa ikiwatatiza kwa muda mrefu hasa wanawake ambao walitembea umbali mrefu kutafuta maji.
“Pamoja na kumalizika kwa kero hiyo, kijiji hicho bado kinakabiliwa na changamoto nyingi za kijamii mojawapo ni ukosefu wa  madaraja yanayowaunganisha na vijiji jirani, zahanati na soko hivyo msituchoke,” alisema Said.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni