Jumatatu, 6 Julai 2015

SILAA AELEZA MAFANIKIO YAKE UKONGA


DIWANI wa Kata ya Gongo la Mboto, Jerry Silaa ameainisha mafanikio aliyoyatekeleza katika kipindi cha miaka mitano tangu achaguliwe kuwa diwani na Meya wa Manispaa ya Ilala.
Akiainisha mafanikio hayo, alisema kwamba ameweza kutimiza ahadi mbalimbali alizokuwa ametoa kwa wakazi wa kata za manispaa ya Ilala.
Katika utekelezaji huo, Silaa alivipatia fedha vikundi vya VICOBA, Genereta, vifaa vya michezo kwa vijana na hati za uthibitisho wa ujenzi wa barabara  zitakazojengwa kwa madiwani.
Silaa ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) alitangaza mafanikio hayo katika mkutano wa hadhara jana uliofanyika katika Shule ya Msingi Kitunda iliyopo Ukonga   ambapo pia aliutumia mkutano huo kutangaza nia ya kugombea ubunge kupitia CCM katika uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. 
Aidha mafanikio mengine yaliyopatikana wakati wa uongozi wake, aliyataja kuwa yapo katika sekta ya elimu, afya, maji na ujezi wa barabara Kata  ya Gongolamboto pamoja na kata zote za Manispaa ya Ilala.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni