Alhamisi, 18 Juni 2015

TWANGA PEPETA WAVURUGANA



BAADHI ya wanamuziki wa Bendi ya The African band ‘Twanga pepeta’ wametishia kuihama bandi hiyo kutokana na kile walichokiita kunyanyaswa na viongozi wa bendi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwa sharti la kutotajwa majina yao, wanamuziki hao walisema kumekuwepo na manyanyaso katika bendi hiyo kwa kuwabagua katika kuwalipa mishahara.
“Tumechoshwa na ubaguzi huu maana kwenye kufanya kazi hatubaguliwi lakini wakati wa kulipwa fedha zetu zinakaa miezi miwili wakati kuna wenzetu wanalipwa mapema,” alisema mmoja wa wanamuziki hao.
Mwanamuziki mwingine alisema wamekuwa wakitengwa hasa kipindi cha malipo kwa kuonekana wengine ni bora kuliko wao.
“Kama familia tunazo wote na kila mtu ana majukumu sasa kwa nini wengine walipwe kwa wakati? Kila mmoja amekuja kutafuta pesa,” alisema.  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni