Jumanne, 16 Juni 2015

KESI YA WAIRANI WALIOKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA YAPIGWA TAREHE



KESI ya madawa ya kulevya yenye thamani ya sh. bilioni 2 inayowakabili watu 13 raia wa Iran jana imeendelea kupigwa tarehe baada ya upande wa jamhuri kudai kuwa upelelezi haujakamilika.
Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya kisutu Thomas Simba, wakili wa serikali Adolf Mkini alidai kuwa upelelezi wa shauri hilo bado unaendelea na kwamba anaiomba mahakama kupanga tarehe nyingine ili kutoa nafasi ya kuendelea na upelelezi.
Hata hivyo hakimu Simba alimtaka wakili wa serikali kuhakikisha upelelezi unakamilika au kutoa sababu iwapo atataka tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi kutokana na kuwa ndio utaratibu mzuri kwani mambo ya kila siku kudai kuwa  upelelezi haujakamilika ni mtindo wa kizamani.  
Washitakiwa katika kesi hiyo ni Mansour Rais, Pohel Mohamed, Rasol Barsh, Gulam Razer, Said Mohamed, Nazir Pack, Mohamed Rafiq, Rahim Marabzay, Salim Kosal, Vari Mahmoud, Razer Rais na Allan Javi.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi itakapotajwa tena Juni 29.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni