MSAJILI wa Vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mutungi
amesema mchakato wa kutafuta
wagombea urais unaoendelea ndani ya vyama hauhusiani na ofisi yake na kuwataka wananchi kuacha
demokrasia ifanye kazi ndani ya vyama
husika.
Akizungumza jijini jana Jaji Mutungi alisema jamii inapaswa
iache kila chama ifanye kazi kwakukuza demokrasia katika mchakato huo wa hatua za awali na
endapo kuna mtu ataenda kinyume na taratibu sheria itaweza kumbana badae
kupitia pingamizi za wananchi.
“Watu wengi walikuwa wakifikiri ofisi ipo kimya na hili suala si kweli,huwa tunawasiliana na
wadau husika kwa mujibu wa taratibu
hatua ya kwenda kwenye public(umma) ni ya mwisho,kama chama kimesajiliwa
tuache demokrasia ifanye kazi yake
mchakato wa ndani ya chama huwa hatuna mamlaka nao,”alisema Jaji
Mutungi.
Alisema ni mapema sana kutoa tathimini ya utekelezaji wa
sheria ya gharama za uchaguzi kwakuwa kwa sasa ofisi hiyo kazi yao ni kuangalia
tu na si vinginevyo muda ukifika watachukua
hatua kwa mujibu wa sheria kwakuzingatia malalamiko ya wahusika.
Alisema sheria ya gharama za uchaguzi madhumuni ina lengo la
kudhibiti matumizi katika chaguzi na vitendo vinavyokatazwa na sheria ya nchi.
Alisema wananchi na wadau wa siasa wanapaswa kuzingatia
sheria ya gharama za uchaguzi na kanuni zake za kikomo cha gharama ili kuondoa
usumbufu badae.
“Natoa tahadhali na angalizo kwa vyama vya siasa na
wanasiasa wasipuuzie sheria na kanuni
hizi zitawaathiri nje na ndani ya chama,wanaweza wakahatarisha uteuzi wao na
chama kisipofuatilia na kupitisha mgombea atawekewa pingamizi harakati zote wanazozifanya zitakuwa hazina
maana,”alisema Jaji Mutungi.
Akizungumzia kuhusu vikundi vya ulinzi na usalama vya ndani
ya vyama Jaji Mutungi alisema sheria ya vyama vya siasa inapiga marufuku vyama
kuanzisha vikundi ambayo vinavyofanya kazi sawa na jeshi na polisi.
Alisema kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa vikundi vya
wanachama vilikuwa na jukumu la kuangalia usalama wa mali za chama bila kupewa mafunzo ya kijeshi na vyeo kama
wanavyofanya sasa.
“Kwa bahati mbaya kutokana na sababu ambazo zinafahamika kwa
vyama vya siasa,vyama hivi vimebadili mfumo,jina,uendeshaji na muelekeo wa
vikundi hivi na kuwa na mfumo wa kijeshi .
Baadhi ya vyama vikaviita vikosi vya ulinzi na usalama wa
vyama(guard) kuanzisha mafunzo maalum ya kujilinda,ukakamavu na kupambana na hata kuwekwa vyeo kama vya
jeshi,jambo hili ni ukiukwaji wa sheria ya nchi hivyo navitaka vyama
vilivyofanya hivyo kuvivunja vikundi mara moja,”alisema Jaji Mutungi.
Alisema katiba ya chama chochote yenye kipengele cha kuwa na
jeshi ndani ni batili na endapo wanataka
mabadiliko ya wanapaswa kufuata taratibu
ikiwemo kushawishi kubadilika kwa sheria hiyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni