MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala imemhukumu kwenda jela miaka
minne, Chacha Nyanchini baada ya
kupatikana na hatia ya kumng’ata sikio na kulimeza ndugu yake ambaye ni Chacha
Kiong’otu maarufu kama Chacha.
Hukumu hiyo ilitolewa juzi mahakamani hapo na Hakimu Mkazi
wa mahakama hiyo, Adelf Sachore baada ya kujiridhisha na hoja za upande wa
mashtaka ambao ulikuwa na mashahidi watano waliotoa ushahidi pasi na kuacha
shaka.
“Ninakuhukumu kutumikia kifungo cha miaka minne baada ya
kupatikana na hatia ya kumng’ata sikio la kutosha na kukimeza kipande cha sikio
cha mlalamikaji huku ukijua fika kuwa kufanya hivyo ni kosa kwa mujibu wa
taratibu za nchi,” alisema Sachore.
Awali kabla ya hukumu hiyo kutolewa wakili wa Serikali,
Chesence Gavyole alidai kuwa hakukuwa nakumbu kumbu za mashtaka ya nyuma dhidi
ya mshtakiwa na hivyo kuiomba mahakama kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa
wote wenye tabia kama hizo za kung’ata wenzao.
Katika utetezi wake juu ya kwanini mahakama isimpatie
adhabu kali, Nyanchini alidsai kuwa anafamilia inayomtegemea na kwamba hakukusudia
kufanya hivyo, hivyo mahakama imsamehe kwa kuwa lilikuwa ni kosa lake la kwanza
utetezi ambao ulitupiliwa mbali.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka ilidaiwa kuwa Februari 12,
mwaka huu katika eneo la Kivule Majohe ndani ya Wilaya ya Ilala Dar es Salaam
alimng’ata na meno sikio la kushoto la mlalamikaji na kukimeza kipande hicho
kwa kile kilichodaiw akuwa kuwa ni ugomvi wa kifamilia.
Mwisho
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni