Jumanne, 6 Desemba 2016

ACT WAFUKUA MAKABURI ATCL



CHAMA cha ACT-Wazalendo kimesema Makaburu walimrubuni Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wakati huo, William Kusila, akasaini mkataba kati ya mikataba ya Alliance Air kwenye karatasi ikiwa na nembo ya wizara bila ya maandishi yoyote na kuwapatia makaburu waende wakajaze maelezo wanayoyataka nchini kwao jambo lililochangia kuitesa Air Tanzania hadi leo. 

hayo yalisema jana na Mwenyekiti wa Chama hicho, Anna MghwiraAnna alipozungumza na waandishi wa habari ambapo alisema miaka ya 1990 viongozi wa Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi kupitia kitendo cha usafiri wa anga waliuza njia(Routes) za ATCL kwa mashirika mengine ya ndege na kuilazimisha ATCL kuingia katika mikataba mibovu ya ushirikiano  na kulifilisi shilika hilo.
“Kwa ujanja kampuni ya Swissport ilianzishwa ikiwa chini ya mkurugenzi wake Esther Maro ambaye alikuwa ni mdogo wake Anna Mkapa, na kulinyang’anya shirika majukumu yake huku Gulf Air, Emirates na Kenya Airways zikiongezewa njia na wakawa waendeshaji wa njia kama mashirika ya Taifa la Tanzania,” alisema Anna.   
Alisema katika awamu ya tatu na nne ATC ilinyang’anywa huduma za chini uwanjani na kulazimishwa kuingia ubia na South African Airways(SAA) na Makaburu hao kuilazimisha menejimenti na bodi ya ATC kupunguza marubani15 na wahandisi 30 kwa kuwadanganya kuuza ndege za kizamani.
“Ndege zilizouzwa aina ya B737-200 zilikuwa zinaruka vizuri kwa safari za ndani na nje zilifika Ulaya, Marekani na Afrka kusini, ambazo zilituwa na makampuni mengi kwa ahadi ya kutuletea za kisasa zenye uwezo wa kusafiri umbali mrefu,” alisema Anna.

aidha kimeishauri serikali kulirudishia Shirika la Ndege la Taifa(ATCL) mamlaka ya kumiliki huduma zote za chini(Ground handling) za uendeshaji wa viwanja vya ndege.
Pia wameiomba serikiali kuunda kitengo cha uwezeshaji ambacho kitahudumia shughuli zote zinazofanyika katika viwanja vya ndege nchini ili kuimarisha usalama wa nchi.
 alisema huduma hizo ni pamoja na huduma kwa abiria, kuhudumia mizigo yote ya Ndege, huduma za vyakula na kambi ndani ya ndege na ukatishaji wa tiketi.
Alisema huduma hizo ni moja ya vitega uchumi muhimu katika mashirika ya ndege ya nchi, Duniani kote kwa kuwa biashara ya ndege haitegemei kuwa na ndege pekee hivyo kutaka maandalizi yaanze mapema ili zikiwasili mfumo wa uzalishaji uko vizuri.
“Kwa kutoa huduma hizi kwa umakini na kuvimilikisha viwanja kwa wananchi wazalendo ambao watakuwa waajiriwa wake, shirika litaweza kuzalisha fedha nyingi na kutoa ajira kwa watanzania,” alisema Anna.
Alisema kwa muda mrefu sasa Tanzania imekwenda kinyume na utaratibu huo jambo ambalo ni kuinyakulia ATCL raslimali zake na hivyo kuinyima mapato.
Alisema ubinafsishaji wa raslimali hizo haukufanyika kwa lengo la kuimarisha usimamizi bali ulichangiwa na tabia ya rushwa ya kupata asilimia kumi ya faida kwa viongozi walioongoza na kulididimiza taifa.
“Uendeshaji wa mifumo ya compyuta,mfumo wa usalama wa viwanja, utunzaji wa mizigo, utunzaji wa abiria, kitengo cha uhandisi na huduma ya kuuza mafuta ya ndege viwe chini ya shirika kwa ajili ya usalama wa nchi na kuzalisha ajira,  kwani ni rahisi kwa wageni kurubuniwa” alisema Anna.
 
     

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni