Jumapili, 15 Januari 2017

E-CONNECT KUTATUA CHANGAMOTO ZA ELIMU


TAASISI ya Econnect imetengeneza mfumo wa kielektroniki wa kukusanya taarifa utakaosaidia kutatua changamoto mbalimbali za elimu nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Hashimu Magesa alisema mfumo huo utasaidia upatikanaji wa takwimu sahihi na kwa wakati zinazohusuidadi ya shule, idadi ya wanafunzi waliopo na walimu.
Alisema mfumo huo ambao tayari umefanyiwa majaribio katika Manispaa ya Ilala utatatua tatizo la mawasiliano kati ya utawala wa shule na wazazi.
“Kwa kutumia mfumo huu shule itakuwa na uwezo wa kutoa taarifa kwa mzazi au mlezi wa mwanafunzi husika ambaye atakuwa hajafika shuleni,” alisema Magesa.
Alisema kwa kutumia mtandao wadau wanaweza kujua mahali shule ilipo, mandhari yake, mawasiliano yake pamoja na historia fupi ya shule hiyo.
“Taarifa zitakazopatikana katika mfumo huo ni orodha ya wanafunzi kwa majina, jinsia, namba za simu za wazazi au walezi, idadi ya wanafunzi waliohama na kuhamiaidadi ya madawati na viti,idadi ya walimu kwa majina jinsia na masomo wanayofundishamuda alioanza kazi, daraja lake kiwangoo cha elimuna namba yake ya simu,” alisema Magesa.
Alisema vingine ni idadi ya walimu waliosataafu, walioko masomoni, idadi ya vyumba vya madarasa, mashimo ya vyoo, compyuta na vyumba vyake, maabara na nyumba za walimu, stoo, maji, umeme na eneo la shule kama limepimwa.

Aidha alitoa wito kwa serikali na wadau wa elimu nchini kuutumia mfumo huo kwa najaribio ndani ya mwaka ili kujiridhisha ufanisi wake.       

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni