Jumanne, 3 Januari 2017

DC AHAMASISHA UTALII KUGAMBONI

MKUU wa Wilaya ya Kigamboni, Hashimu Mgandilwa amewataka wananchi wa Dar es Salaam kuondoa dhana kuwa Fukwe zote za wilaya hiyo ni za kulipia.
Akizungumza muda mfupi baada ya kufanya usafi katika maeneo ya fukwe, Mgandilwa alisema eneo la ufukwe wa Bahari ya Hindi ni   mali ya umma hivyo wasiogope kwenda kutembelea. 
Alisema kwa mujibu wa sheria eneo lililopo ndani ya mita 60 kutoka kingo za bahari ni mali ya umma na hakuna mwenye mamlaka nayo isipokuwa serikali.
“Changamoto iliyopo hapa ni ukosefu wa njia za kuingilia ambapo kwa sasa kuna njia zipo wazi na nitakutana na wizara ya Maliasili na Utalii kuangalia namna ya kuweka njia zaidi za wananchi kuingia,” alisema Mgandilwa.
Aidha amewakikishia usalama wananchi na wageni watakaokwenda kutembelea katika fukwe hizo.
“Tumefanya usafi kama kuhamasisha utalii wa ndani na nje katika eneo hili kwa kuwa sasa ni sehemu ya utalii wa jiji la Dar es Salaam,” alisema Mgandilwa.
Mgandilwa alivitaja vivutio mbalimbali vilivyopo katika wilaya hiyo kuwa ni mbuyu wenye umbo la chupa ya shampeni, visiwa sita kikiwamo cha Sinda chenye mazalia ya kasa, jengo kale lililojengwa na Wajerumani. 
Aliwashukuru wanamuziki waliotoka nje na ndani ya nchi kushiriki usafi na kuhamasisha utalii wa Kigamboni.
 “Uwepo wenu hapa utaihamasisha jamii na kuitangaza Tanzania kim,ataifa,” alisema.
Naye mwanamuziki wa miondoko ya kufokafoka kutoka Marekani,Akua Naru alisema amefarijika kushiriki usafi wa fukwe na kuchangia kutoa elimu ya utalii kwa watanzania.
“Tutaitangaza vema nchi hii kwa kuwa na fukwe nzuri na utulivu mkubwa hasa kwa sisi wasanii kufanya shughuli zetu,” alisema Akua.
Naye Fred Maliki(Mkoloni) kutoka katika kundi la wagosi wa Kaya alisema amefurahi kuanza mwaka akiwa na jamii.
“Kushiriki kufanya usafi kwa vijana ina maana tunajitambua na tunaweza kuhasisha utalii kwa Wilayah ii,” alisema Mkoloni.

mwisho 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni