Alhamisi, 5 Januari 2017

DC Awaonya mafataki

MKUU wa Wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga amewaonya wanaume wenye tabia ya kufanya mapenzi na wanafunzi kuwa hawatasalimika na mkono wa sheria.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara wa wananchi katika kata ya Mipeko, Sanga alisema wanaume wenye tabia hizo kama hawatabadilika wataishia magerezani.
“Nyinyi wanaume acheni kutamani wanafunzi na muwaogope sana maana sheria haitawaacha salama,” alisema.
Alisema katika mwaka huu anawaomba watoto wote wanaotakiwa kwenda shule wapelekwe ili kukinusuru na ujinga kizazi hicho.

“Watoto wanaotakiwa kwenda darasa la kwanza waende na waliofaulu kwenda kidato cha kwanza waende atakayeshindwa kumpeleka mwanaye shule hatua kali za sheria dhidi yake zitachukuliwa,” alisema Sanga.  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni