TAASISI ya Econnect imetengeneza mfumo wa kielektroniki wa
kukusanya taarifa utakaosaidia kutatua changamoto mbalimbali za elimu nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es
Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Hashimu Magesa alisema mfumo huo
utasaidia upatikanaji wa takwimu sahihi na kwa wakati zinazohusuidadi ya shule,
idadi ya wanafunzi waliopo na walimu.
Alisema mfumo huo ambao tayari umefanyiwa majaribio katika
Manispaa ya Ilala utatatua tatizo la mawasiliano kati ya utawala wa shule na
wazazi.
“Kwa kutumia mfumo huu shule itakuwa na uwezo wa kutoa
taarifa kwa mzazi au mlezi wa mwanafunzi husika ambaye atakuwa hajafika
shuleni,” alisema Magesa.
Alisema kwa kutumia mtandao wadau wanaweza kujua mahali
shule ilipo, mandhari yake, mawasiliano yake pamoja na historia fupi ya shule
hiyo.
“Taarifa zitakazopatikana katika mfumo huo ni orodha ya
wanafunzi kwa majina, jinsia, namba za simu za wazazi au walezi, idadi ya
wanafunzi waliohama na kuhamiaidadi ya madawati na viti,idadi ya walimu kwa
majina jinsia na masomo wanayofundishamuda alioanza kazi, daraja lake kiwangoo
cha elimuna namba yake ya simu,” alisema Magesa.
Alisema vingine ni idadi ya walimu waliosataafu, walioko
masomoni, idadi ya vyumba vya madarasa, mashimo ya vyoo, compyuta na vyumba
vyake, maabara na nyumba za walimu, stoo, maji, umeme na eneo la shule kama
limepimwa.
Aidha alitoa wito kwa serikali na wadau wa elimu nchini
kuutumia mfumo huo kwa najaribio ndani ya mwaka ili kujiridhisha ufanisi wake.