Jumatano, 28 Septemba 2016

majengo kale yahofiwa kupotea

IDADI ya majengokale katika jiji la Dar es Salaam yanahofiwa kupotea kutokana kukua kwa kasi kwa jiji hilo.
Akizungumza katika kongamano la urithi na uhifadhi wa majengo kale, Mkurugenzi wa Kituo cha Urithi na ubunifu Majengo Dar es Salaam, Aida Mulokozi alisema mpaka sasa majengokale yanayotambuliwa na serikali ni 25 tu.
Alisema sura ya jiji hilo imebadilika kutokana na ukuaji wa kasi hivyo kutishia urithi wa kihistoria wa majengokale.
“Leo Dar es Salaam ni miongoni mwa majiji kumi yanayokuwa kwa haraka zaidi Duniani kutokana na shinikizo la uchumi maslahi ambayo yanayogongana na mamlaka dhaifu hivyo urithi wake uko katika hatari ya kupotea.
“Kasi ya maendeleo ni kubwa na kubasababisha mabadiliko ya haraka huku majengo mengi ya kihistoria kuvunjwa,” alisema Aida.
Alisema anaishauri serikali kuanzisha sheria itakayozuia majengo ya kale kubomolewa na kuachwa kama kumbukumbu.
“Kuna faida kubwa za majengo kale kama wizara ya ,aliasili na utalii wakiwekea mkazo wa kuyahifadhi na kuyatangaza,” alisema Aida.
Alisema moja ya faida kubwa ni kuongeza vivutio vya watalii ambao wengi hupenda kutembelea majengo ya kale.

“Majengo kale yamekuwa yakitumika vema kule Zanzibar kwani yamekuwa yakiingiza theruthi mbili ya pato la taifa,” alisema Aida.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni