HOSPITALI
ya Aga khani inatarajia kufanya upasuaji bure kwa wanawake na watoto walioungua na kushindwa
kuvitumia baadhi ya viungo hivyo wenye matatizo hayo wafike Disemba 12, mwaka huu katika hoptali ya Dar es Salaam.
Akizungumza
na FICHUA, Ofisa Mawasiliano wa hospitali hiyo, Edna Mullumba alisema upasuaji
huo utafanywa na jopo la madaktari wa kike kutoka nchi mbalimbali.
“Upasuaji
huo utafanywa kwa wanawake na watoto wa jinsia ya kike tu kwa kuwa mradi huo
unaitwa Women to women hivyo watoto wa kiume watatibiwa kwa sababu za msingi
tu,” alisema Edna.
Alisema
wagonjwa hao watafanyiwa upasuaji na kuweza kuvitumia viungo ambavyo viliungua.
Alisema
matibabu hayo yatahusisha makovu yatokanayo kwa kuungua moto na kusababisha
sehemu ya mwili kushindwa kutumika kama mkono, kiwiko na bega.
“Watatibiwa
pia walioungua sura na kukwamisha uwezo wa mwanamke kufumba na kufumbua macho,
kufungua na kufunga mdomo pamoja na kugeuza shingo ama kichwa,” alisema Edina.
Alisema
yatatibiwa pia majeraha ya miguu yanayosababisha mgonjwa kushindwa kutembea ama
kutembea kwa shida kuungua sura na kuungua kifua.
mwisho
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni