Jumanne, 1 Desemba 2015

WALIOUNGUA MOTO KUTIBIWA BURE



HOSPITALI ya Aga khani inatarajia kufanya upasuaji bure kwa  wanawake na watoto walioungua na kushindwa kuvitumia baadhi ya viungo hivyo wenye matatizo hayo wafike Disemba 12, mwaka huu katika hoptali ya Dar es Salaam.
Akizungumza na FICHUA, Ofisa Mawasiliano wa hospitali hiyo, Edna Mullumba alisema upasuaji huo utafanywa na jopo la madaktari wa kike kutoka nchi mbalimbali.
“Upasuaji huo utafanywa kwa wanawake na watoto wa jinsia ya kike tu kwa kuwa mradi huo unaitwa Women to women hivyo watoto wa kiume watatibiwa kwa sababu za msingi tu,” alisema Edna.
Alisema wagonjwa hao watafanyiwa upasuaji na kuweza kuvitumia viungo ambavyo viliungua.
Alisema matibabu hayo yatahusisha makovu yatokanayo kwa kuungua moto na kusababisha sehemu ya mwili kushindwa kutumika kama mkono, kiwiko na bega.
“Watatibiwa pia walioungua sura na kukwamisha uwezo wa mwanamke kufumba na kufumbua macho, kufungua na kufunga mdomo pamoja na kugeuza shingo ama kichwa,” alisema Edina.
Alisema yatatibiwa pia majeraha ya miguu yanayosababisha mgonjwa kushindwa kutembea ama kutembea kwa shida kuungua sura na kuungua kifua.
mwisho   

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni