WAFANYAKAZI
wa serikali wa mkoa wa Dar es Salaam wameahidiwa kujengewa nyumba katika
viwanja vyao ili kuondokana na kero za kodi za nyumba.
Akizungumza
katika maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi ilivyofanyika kimkoa jijini Dar es
Salaam Mkuu wa Mkoa wa huo, Paul Makonda alisema wafanyakazi wamekuwa wakipata
taabu nyingi kutokana na mishahara kutokidhi mahitaji ya kodi za nyumba na
gharama za maisha.
Alisema
mishahara wanayopata haiwezi kutosha kuhimili mazingira ya maisha ya jiji la
Dar es Salaam.
“Sisi kama
serikali ya mkoa tumekaa na kufikiri kuona namna ya kutafuta watu
watakaowajengea nyumba ndani ya miezi sita katika viwanja vyenu nanyi mtalipa
taratibu,” alisema Makonda.
Alisema
tayari wamenza kutengeneza baadhi ya ramani ambazo wafanyakazi hao watachagua
wanazozitaka.
“Mtalipa
taratibu kwa kuwa nyinyi ni watumishi wa umma na mimi kama mkuu wa mkoa
nitawadhamini,” alisema Makonda.
Aliongeza
kuwa katika hatua za uboreshaji wa mazingira ya kufanyia kazi wameanza na
walimu ambao ni kundi kubwa kwa kuwawezesha kusafiri bure.
“Lengo langu
halikuwa kuishia katika usafiri wa daladala bali utasaidia hata katika mabasi
yaendayo kasi japo nilisikitika sana kusikia baadhi ya viongozi wenu kutoa
kauli ya kukataa eti kwa sababu wanadai wanamalimbiko na nyongeza ya mishahara.
Leo umenikuta
mwenge unaniomba nauli ya kwenda posta kwa daladala mimi nakwambia nina gari unaanza kutoa sababu za kuwa huna
chakula,” alisema Makonda.
Aidha
alisema katika kuhakikisha jiji la Dar es Salaam wanatarajia kuachana na
matumizi ya mifuko ya plastiki maarufu kama Rambo.
“Niwaombe
viwanda wanaotengeneza mifuko hiyo watubadilishie mifuko hii wa ndani ya siku
90,” alisema Makonda.
Awali
akisoma Risala kwa mgeni Rasmi, Mratibu wa maadhimisho hayo, Elias Chizingwa
alisema wafanyakazi wa mkoa huo wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwamo
mishahara duni isiyokidhi mahitaji hasa katika jiji la Dar es Salaam,
wafanyakazi kukatwa kodi mara tatu, baadhi ya waajiri kuchelewesha kupeleka
michango katika mifuko ya hifadhi za jamii.
“Changamoto
nyingine ni mazingira magumu ya kufundishia walimu, baadhi ya waajiri
kutokuvitambua vyama vya wafanyakazi na baadhi ya makampuni ya wawekezaji wa
nje kuwanyanyasa wafanyakazi wazalendokwa kuwafanyisha kazi kwa masaa zaidi 18,”
alisema Chizingwa.
mwisho
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni