Jumapili, 25 Februari 2018

tumieni bidhaa za viwanda vya ndani

na tunu nassor



WATAALAMU wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji wameshauriwa kutumia bidhaa zinazozalishwa nchini katika kutekeleza miradi ya maji ili nchi kuangalia mikataba wanayoingia ili nchi inufaike na miradi hiyo.
Akizungumza katika ziara aliyoifanya jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso alisema wataalamu hao waangalie mikataba wanayoingia ili kuruhusu baadhi ya vifaa vya ujenzi kununuliwa nchini.
Alisema kwa sababu nchi hii kwa sasa ni ya viwanda hivyo ni vyema wanapoingia mikataba kuondoa vipengele vitakavyowafunga katika kununua baadhi ya vifaa.
"Si busara vifaa kama koki na pampu kununuliwa nje ya nchi wakati vinapatikana hapa nchini,” alisema Aweso.
Alisema kwa kufanya hivyo kutasaidia kuongeza mitaji katika viwanda vya ndani, ajira na kuongeza mzunguko wa fedha nchini.
"Pamoja na kuwa na nia njema ya kuwapatia wananchi maji safi na salama lakini pia waliangalie hili kwa manufaa ya nchi,” alisema Aweso.
Aidha aliongeza kuwa bado kuna changamoto ya kuwapo kwa makandarasi wasiokidhi vigezo ambao hutekeleza miradi chini ya kiwango.
“Bado tuna changamoto ya makandarasi wanaopewa miradi 'kiushemeji shemeji' jambo ambalo linasababisha kushindwa kuteteleza kwa kiwango hivyo kama wizara tutawatapisha fedha hizo na kuzirudisha katika miradi," alisema Aweso.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi kutoka Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam(Dawasa), Modester Mushi alisema wanatarajia kuwaunganishia maji wateja 376,000 katika visima vya Mpera na Kimbiji.
Mwisho

dawasa, dawasco pelekeni maji pembezoni mwa mji


Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso ameziagiza DAWASA na DAWASCO kuhakikisha zinafikisha huduma ya maji kwenye maeneo yaliyo pembezoni mwa Jiji la Dar es Salaam, ambapo kuna uhaba mkubwa wa maji pamoja na kuwa na wakazi wengi zaidi na si kujikita katikati ya jiji hilo tu.Naibu Waziri Aweso ametoa agizo hilo akiwa katika ziara ya kikazi katika Wilaya ya Temeke kujionea uhalisia wa utekelezaji wa miradi ya maji, wilaya ambayo imekuwa na malalamiko mengi kuhusiana na huduma hafifu ya majisafi  na salama.Aweso amesema kuwa kuna haja ya DAWASA na DAWASCO kuimarisha huduma ya maji kwenye maeneo ya pembezoni mwa jiji kama Temeke, Kigamboni, Ukonga, Mbagala na Segerea ili kukidhi mahitaji makubwa ya maji kwa wakazi wengi wanaoishi maeneo hayo.''Fanyeni utaratibu wa kukarabati miradi ya zamani kama hatua ya kwanza na ya haraka ya kuwapatia wananchi maji, wakati mkiendelea kutekeleza miradi mipya na mikubwa ambayo utekelezaji wake utachukua muda mrefu. Mmejikita sana katikati ya jiji, ambapo kwa sasa huduma hiyo imeimarika kwa kiasi kikubwa. Umefika wakati wa kuwekeza maeneo ya pembezoni kwa sasa, na wakazi hawa nao wafurahie huduma ya maji ya uhakika'', aliagiza Naibu Waziri Aweso.Aidha, Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji alitoa onyo kwa manispaa zote za Jiji la Dar es Salaam kutowapa kazi wakandarasi wasio na uwezo. Pia, kuchukua hatua stahiki kwa wakandarasi wote wanaosuasua katika utekelezaji wa miradi, huku akiwahakikishia wakandarasi wote kulipwa fedha zao kwa wakati ili wasikwame katika