Jumatatu, 16 Oktoba 2017

ushahidi wa tatu watua takukuru

Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema) amewasilisha ushahidi mwingine kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU

Madiwani hao nane wa Chadema wamejiuzulu kwa kile walichoeleza kumuunga mkono Rais John Magufuli jambo ambalo Nassari anadai siyo kweli bali walinunuliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo nje ya ofisi ya Takukuru Upanga jiji ni humo alisema huu ni ushahidi wa tatu na kadri upepelezi ukiwa unaendelea ataleta mwingine, kwani ni kama filamu ya Isidingo.

Nassari alisema alitarajia Rais Dk. John Magufuli angewachukulia hatua wateule wake wanaohusishwa katika sakata hilo ili kupisha uchunguzi uweze kufanyika kwa uhuru.

"Tunajiuliza kwa nini Rais hawachukulii hatua DED, DAS au DC wote wa Arumeru kwa kutuhumiwa, watupeleke mahakamani na tungeomba suala hili lichukuliwe kwa uzito wake," alisema Nassari

Naye Mbunge wa Ubungo, Saed Kubunea aliyeongozana na Nassari alisema ameshiriki kuwashauri kuutoa ushahidi huo kwa umma ili jamii ijue ukweli.
"Tunachojiuliza kwa nini rais yupo kimya, kwa nini mawaziri na viongozi waliotuhumiwa Katika sakata la Almas na Tanzanite aliwasimamisha kwa nini hawa hataki," alihoji Kubenea