Jumatano, 1 Juni 2016

KUMEKUCHA MISS SINZA



WAREMBO wenye sifa katika kitongoji cha Sinza wametakiwa kujitokeza kuchukua fomu za shindano la kumtafuta mrembo wao ‘Miss Sinza’ litakalofanyika Julai 29 mwaka huu.
Akizungumza na Waandishi wa habari jana Mratibu wa shindano hilo Robert Majaliwa alisema kitongoji hicho hakifanya mashindano hayo katika mwaka uliopita kutokana na kufungia Miss Tanzania .
Alisema wanataka fomu za kujiunga wafike katika Ofisi za kamati ya maandalizi Rona Promotion & Enterteinment zilizopo Sinza Mapambano.
“Sehemu nyingine ni katika ofisi za Miss Tanzania zilizopo mikocheni, Ofisi za Miss Kinondoni, Shear Ellusion na Defrance Hotel” alisema Majaliwa.
Pamoja na hivyo Majaliwa aliwaomba wadau mbalimbali kujitokeza kudhamini shindano hilo.