WAREMBO
wenye sifa katika kitongoji cha Sinza wametakiwa kujitokeza kuchukua fomu za
shindano la kumtafuta mrembo wao ‘Miss Sinza’ litakalofanyika Julai 29 mwaka
huu.
Akizungumza
na Waandishi wa habari jana Mratibu wa shindano hilo Robert Majaliwa alisema
kitongoji hicho hakifanya mashindano hayo katika mwaka uliopita kutokana na
kufungia Miss Tanzania .
Alisema
wanataka fomu za kujiunga wafike katika Ofisi za kamati ya maandalizi Rona
Promotion & Enterteinment zilizopo Sinza Mapambano.
“Sehemu
nyingine ni katika ofisi za Miss Tanzania zilizopo mikocheni, Ofisi za Miss
Kinondoni, Shear Ellusion na Defrance Hotel” alisema Majaliwa.
Pamoja na
hivyo Majaliwa aliwaomba wadau mbalimbali kujitokeza kudhamini shindano hilo.